Wapendwa ndugu zangu nachukua fursa hii kuwasalimu kwa siku ya leo ambayo tumepata Neema ya kukuta. Kuna siku niliwaahidi kuwa nitawaletea picha za usiku wa mkesha. Sasa wakati na siku imefika ya kuwaonesha kwa sehemu kupitia picha za mnato. na tukipata nafasi utaweza kuiona tena kwa kupitia njia ya video.
Mtumishi wa Mungu Dada Marther akitibua wingu la sifa. Haaaaa, ilikuwa ni balaa kwelikweli,tulimwona El Shadai kwa kiwango cha juu sana. Hata kama ulikuwa hutaki kusamama na kumsifu Mungu ungejikuta ukiamka mwenyewe bila kupenda.
Na hapo Mtumishi wa Mungu Dada Assia alikuwa akumtumikia Mungu kwa namna ambaya Mungu alimuwezesha kuyafanya. Kwa kweli Tulimwona Mungu kwa Namna ya ajabu.
Watumishi wa Mungu wapigaji vyombo walifanya mambo ya ajabu sana na kumdhihirisha Mungu kupitia kipawa walichopewa na Mungu wao. Kwa kweli drums zilitulia,guitor la base lilikuwa linaleta utamu hasa, bila kuvisahau vinanda viwili vilivyo leta ladha nzuri tofautitofauti