Tuesday, November 13, 2012

"SI LAZIMA WAENDE ,WAPENI NINYI CHAKULA" MATHAYO 14:13-21

UTANGULIZI
   " SI LAZIMA WAENDE, WAPENI NINYI CHAKULA" Ni maneno ya Bwana Yesu alipokuwa akiwaambia wanafunzi wake wakati alipokuwa na makutano makubwa ya watu waliomfuata katika faragha na faragha hiyo ilifanyika nyikani, mahali ambapo hapakuwa na chakula, na hali wakiwa katika mfungo wa siku ya tatu. Hiyo siku ya tatu walikuwa na njaa na ndipo wananafunzi wakamwambia Yesu kuwa watu wana njaa unaonaje waende wakanunue vyakula, ndipo Yesu akawaambia wapeni ninyi chakula, ndipo wakajibu hatuna ila tuna SAMAKI WAWILI  NA MIKATE MITANO TU.
   Kwa mtumishi wa Mungu ni lazima kuwa na chakula cha akiba mda wote. Akiba ya chakula ni kwa ajili ya kundi la Bwana. Kwani ukiwa mtumishi katika eneo lolote lile ulilopewa na Mungu jua kuwa watu wa eneo hilo wako chini yako. Kutegemea kwao kunategemea sana na wewe umekaaje na sheria ya Bwana. MALAKI 2:7 "Kwa maana yapasa midomo ya kuhaniihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake (mtumishi wa Mungu) kwa kuwa yeye ni mjumbe wa Bwana waMajeshi"
     Hivyo kama Mtumishi wa Mungu ni wajibu wako kutafuta chakula kwa ajili ya eneo lako na si chakula tu bali pia kiwepo chakula cha akiba . Mtu akija kwako akiomba chakula inakubidi uumpe haijalishi unacho au hauna your responsible to give him/her. Kwanini? kwa sababu eneo unalopewa na Mungu anakupa chakula cha kutosha kwa kipindi fulani, na kama amekupa hiyo kwa kipindi hicho unatakiwa pia kuwa na akiba ya dharura. Ndha unafahamu nini maana ya dharura. Dharura jambo linalo tokea lisiloterajiwa katika sehemu hiyo bila kuwa na wakati maalum,sehemu maalum taarifa maalum. Kwa mfano ukipokea mshahara ukapanga bajeti yako, na ukanunua kila kitu ndani, halafu unakuta hujabakiwa na kitu ndani, ghafla unashangaa kumetokea msiba kijijini uliko zaliwa halafu kijiji hicho na takribani kilometa 700, halafu wewe ni wa muhimu sana katika msiba huo na ukiangalia mfukoni huna fedha, hatimaye unaishia kukopa. Ndivyo hata ulimwengu wa Roho kulivyo. Mungu akikupa chakula kwa ajili ya watu wa eneo lako, anakupa  kwanza akili ya kuweza kukitumia chakula hicho, kwani chakula ni cha wakati na wakati. Leo hii ukimpa chakula kisicho cha wakati mtu atakiona kuwa hakimfai  kwa nini? ukisoma MHUBIRI 3:1 " Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu" Kwa hiyo inatakiwa kuwa na chakula cha wakati na cha akiba pia.
ITAENDELEA..........

Friday, November 9, 2012

MABADILIKO YA BLOG HII KIMWONEKANO

HABARI NDUGU ZANGU.
      NAFIKIRI MTAKUWA MMEONA MABADILIKO YALIYO TOKEA KATIKA BLOG YETU. KAMA UNA MAONI YOYOTE BASI TUANDIKIE KUPITIA UKURASA WETU WA FACEBOOK   . lusajo media production. NA KAMA UMEIPENDA BASI BOFYA KATIKA KITUFE CHA "LIKE". 
      NI KUTOKANA NA MAENDELEO YA KI-TEKNOLOJIA. SASA UNAWEZA KUPATA HABARI HIZI KUPITIA LUGHA MBALIMBALI DUNIANI. 

      KILICHO BAKI NI KUTUOMBEA!!!!!!

Wednesday, September 19, 2012

MKESHA WA KUSIFU NA KUABUDU

Wapendwa ndugu zangu nachukua fursa hii kuwasalimu kwa siku ya leo ambayo tumepata Neema ya kukuta. Kuna siku niliwaahidi kuwa nitawaletea picha za usiku wa mkesha. Sasa wakati na siku imefika ya kuwaonesha kwa sehemu kupitia picha za mnato. na tukipata nafasi utaweza  kuiona tena kwa kupitia njia ya video.

Mtumishi wa Mungu Dada Marther akitibua wingu la sifa. Haaaaa, ilikuwa ni balaa kwelikweli,tulimwona El Shadai kwa kiwango cha juu sana. Hata kama ulikuwa hutaki kusamama na kumsifu Mungu ungejikuta ukiamka mwenyewe bila kupenda.
Na hapo Mtumishi wa Mungu Dada Assia alikuwa akumtumikia Mungu kwa namna ambaya Mungu alimuwezesha kuyafanya. Kwa kweli Tulimwona Mungu kwa Namna ya ajabu.
  
Watumishi wa Mungu wapigaji vyombo walifanya mambo ya ajabu sana na kumdhihirisha Mungu kupitia kipawa walichopewa na Mungu wao. Kwa kweli drums zilitulia,guitor la base lilikuwa linaleta utamu hasa, bila kuvisahau vinanda viwili vilivyo leta ladha nzuri tofautitofauti

Friday, September 14, 2012

Tuesday, September 11, 2012

WAPENDWA WOTE MLIOSHIRIKI KATIKA MKESHA

WA KUSIFU NA KUABUDU.

 

Tunapenda kuwashukuru watu wote mlio ungana nasi katika mkesha wa kusifu na kuabudu uliofanyika katika kanisa la Lutheran usharika wa Ruanda,Jimbo la Mbeya iliyopo Dayosisi ya Konde. Kwa kweli tuliona Utukufu  wa Bwana ukishuka kwa namna ya ajabu sana. Mungu  awabariki.

Skukrani zetu ziwaendee watu woye waliofanikisha shughuli nzima ya maandalizi.

Kamati ya Maandalizi kwa ujumla chini ya Mwenyekiti wake Ndg TUNTUFYE ARNOLD.

Ndugu wanavyuo wote waliojitoa kwa ajili ya maandalizi yote.

Ndugu wote waliotoka nje ya mkoa kwa ajili ya maandalizi na kuhudhuria.

Pia kwa watu wote walio jitokeza kuungana nasi kwa pamoja ili Tulitukuze Jina la Bwana,MUNGU AWABARIKI. 

Mungu akitupa uzima siku si nyingi mtaziona picha zilizopigwa wakati wa kusifu na kuabudu,mtuwie radhi ni kutoka na sababu zilizopo juu ya uwezo wetu tumeshindwa kuwaletea picha hizo.

Wednesday, August 22, 2012

LUSAJO MEDIA PRODUCTION  wakishirikiana na YOUTH CHRISTIAN UNION, wanakuletea   u siku wa concert kubwa ya kusifu na kuabudu itakayofanyika katika kanisa la KKKT-USHARIKA WA RUANDA.
Ni usiku wa Ijumaa kuamkia Jumamosi ya Tarehe ya 7/Septemba/2012. Nyote mnakaribishwa katika concert hiyo na Mungu awabariki

Monday, July 30, 2012

KARIBU MBEYA

KARIBUNI NYUMBANI KARIBUNI MBEYA

VIDEO PRODUCTION

PHOTO SHOP, PRINTING AND PUBLISH



KARIBU TUWE PAMOJA KATIKA KUENDELEZA UBORA WA KAZI ZA DIGITAL, eg PICHA, VIDEO NA HATA SAUTI PIA........ WASILIANA NASI UTUPI DHAMANA YA KUKUFANYIA KAZI YENYE KIWANGO CHA KIMATAIFA 

LUSAJO MWAIHABI
C.E.O
LUSAJO MEDIA PRODUCTION