Makala yetu (ICT)



 COMPUTER IMETOKEA WAPI?

Mpenzi Msomaji wa Blog hii nakukaribisha sana katika Makala yetu ya Kwanza kabisa inayoelezea maisha ya Computer tokea kipindi inavumbuliwa mpaka leo tunaitumia. Hii ni historia ya Computer iliyopo katika kumbu kumbu mbali mbali za kimtandao na vitabuni. Hivyo nakukaribisha sana usome na uelewe ili tunako elekea kusiwe kugumu sana

Kompyuta ilijulikana kwa mara ya kwanza mnamo karne ya 19 kupitia Profesa jina lake aliitwa Prof CHARLES BABBAGE  alikuwa ni Mwangereza na alikuwa mtaalamu wa Hesabu, Mwanafalsafa, Mhandi wa Mitambo ( Mechanical Engineer) na ndiye aliyeleta wazo la kompyuta.
Unapozungumzia kompyuta unazungumzia hatua tatu au Vizazi vikuu vitatu. Na kila hatua ina Miaka yake na Maendeleo ya Kiteknolojia.
 Prof. Charles Babbage

KIZAZI CHA KWANZA (1937-1946)
Mnamo mwaka 1937 Computer ya kwanza ilitengenezwa na  Dr John V. Atanasoff na Bw Clifford Berry. Na Computer hii iliitwa ATANASOFF-BERRY COMPUTER (ABC).

 Fig 1. ATANASOFF-BERRY COMPUTER (ABC).

Mnamo mwaka 1943, Computer iitwayo COLOSSUS ilijengwa na wanajeshi
 

 Fig 2. COLOSSUS COMPUTER


Maendeleo madogo madogo yaliendelea na ikiwa lengo hasa ni kutengeneza Computer kubwa iliyoitwa ELECTRONIC NUMERICAL INTERGRETOR AND COMPUTER (ENIAC).
 Fig 3. ELECTRONIC NUMERICAL INTERGRETOR AND COMPUTER (ENIAC).

*Computer hii ilikuwa na uzito wa Tani 30
*Ilikuwa na vacuum Tubes 18,000 ambazo zilikuwa zinafanya kazi
* Kwa mara ya kwanza hii computer ilianza kwa kutoa mwanga hafifu sana
*Na computer hii iliweza kufanya kazi moja tu na haikuwa na Operating System (Windows 7, Windows XP n.k)



KIZAZI CHA PILI CHA COMPUTER (1947-1962)
Katika kipindi hiki au kizazi hiki cha pili cha computer, Computer zilikuwa zikitumia zaidi TRANSISTOR badala ya VACUUM TUBES kwa sababu ziliaminika zaidi.

Mnamo mwaka 1951, Computer ya kwanza kwa ajili ya biashara, iligunduliwana kutangaza kwa jamii. Na computer hi iliitwa UNIVERSAL  AUTOMATIC MAC HINE (UNIVAC 1).

Fig 4. UNIVERSAL  AUTOMATIC MAC HINE (UNIVAC 1).

 
Mnamo mwaka1953, Shirika  lakimataifa linaloshughulikia Mashine za kibiashara, International Business Machine (IBM) lilitengeneza computer ambazo ziliitwa IBM 650 na 700.

Fig 5. IBM 650 computer
Fig 6. IBM 700 computer

Katika kipindi hiki lugha za kitaalamu za kikompyuta (Programming Language)zilikuwazimekwisha tengenezwa zaidi ya 100
                *Computer hizi zilikuwa na kitunza kumbu kumbu(Memory Drive)
                *Computer hizi zilikuwa na Operating System (Windows kwa lugha inayo fahamika sana)
                *Na katika kipindi hiki zilikuja teknolojia za Printer na Tape kwa ajili ya kuhifadhi kumbu kumbu   hifadhiwa. (Hard Copies)



KIZAZI CHA TATU CHA COMPUTER (1953-LEO).

Kutokana na maendeleo makubwa na ubunifu wa hali ya juu sana,Computer iliendelea kupunguzwa ukubwa wa kimwonekano, kutoka  ukubwa wa jengo mpaka computer ya kubebwa kiganjani. Computer za sasa Zina uwezo mkubwa sana ukilinganisha na computer za kipindi kile, zinaweza kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja.

Mnamo mwaka 1980, Microsoft ilizaliwa na kuleta operating system iliyokuwa ikiitwa Microsoft Disk Operating System (Ms DOS)

Mnamo mwaka 1981, IBM alitangaza computer za kutumia maofisini na majumbani ambayo iliitwa Personal Computer (PC)

Mnamo mwaka 1984, Apple alileta Computer iliyoitwa Macintosh PC

Na mwaka 1990 Microsoft ilizindua Operating System iliyoitwa WINDOWS ambayo asilimia kubwa ndiyo inayotumika sana maofisini, majumbani,  nah ii operating system huongezwa ubora kila baada ya kipindi Fulani. Hii ni kutikana na kuzidi kugundulika zaidi kwa teknolojia mpya.

Mpenzi Msomaji wangu anatumaini nitakuwa nimekupa mwanga japo kwa ukaribu, ili uweze kupata picha ya wapi computer ilitokea. Kwa maswali zaidi, maoni , ushauri tupigie namba hizo juu.

Imeandaliwa na 

Lusajo Mwaihabi
mwaihabilusajo@yahoo.com

No comments:

Post a Comment