Mkuu wa shule, Shule ya Sekondari Mwakaleli iliyoko wilaya ya Busokelo Mbeya anapenda kuwakaribisha wanafunzi wote waliochaguliwa katika shule hii.
Monday, July 6, 2015
Monday, June 29, 2015
JOINING INSTRUCTION YA MAWENI SEKONDARI, MBEYA
Maweni Sekondari ni shule ya Serikali kidato cha kwanza hadi cha site mkoani Mbeya. shule ilianzishwa 2006.
Shule ipo katika jimbo la Songwe, katika wilaya mpya inayotarajiwa ya Songwe kwa sasa ni Chunya. Ili kufika Maweni Sekondari panda mabasi yanayo patikana katika mji mdogo wa Mbalizi uliopo Magharibi na nje kidogo ya Jiji la Mbeya (njia ya Tunduma).
Kwa sasa shule ina wanafunzi 1200. wakiwemo 500 kidato cha tano na sita na 700 wa kidato cha kwanza hadi cha nne.
Kwa A level michepuo iliyopo ni CBG, HGE, HGK, HKL, HGL na EGM.
Karibu sana Maweni Sekondari.
Kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0754 603 777
Mkuu wa Shule.
N.B Malipo yote yafanyike katika Account No 60706600135 (NMB) hii.
Friday, August 1, 2014
HARUSI YA EV. JOHN NA SEHEWA
LUSAJO MEDIA PRODUCTION inakuletea Harusi ya Mtumishi wa Mungu Ev. John na Sehewa Chinyuli iliyofanyika katika Kanisa la Anglican Ukonga Mazizini mnamo Tarehe 26 Julai 2014. Na baadae katika ukumbi wa Moshi, Ukonga.
Mr & Mrs John Chinyuli wakiwa katika uso wa furaha baada ya kufunga harusi
Wasimamizi wa Maharusi wakiwa katika hali ya Furaha kubwa baada ya kuwasindikiza ndugu zao
Kulikamilika kupita maelezo
Sherehe iliongozwa kwa umahiri mkubwa sana wenye mitikisiko ya furaha, chini ya MC JEMIMA
Hawa ndugu walikuwa na furaha isiyokuwa na kifani kwa maana hawakuamini kama siku hii yao maalum imefika na kufanikiwa kwa sehemu kubwa sana.
Yaaaani hapo John anasema ubachela bai bai
Akishuka kwa unyenyekevu mkubwa.
CEO wa Lusajo Media Production (katikati) akiwa pamoja na maharusi kwa furaha kubwa wakati sherehe zikiendelea.
Ahsante kwa kuchagua LMP kwa kazi zenye ubora zaidi.
LUSAJO MEDIA PRODUCTION tunawatakia Heri ya maisha mema na Mungu wetu wa Mbinguni na awabariki sana.
Subscribe to:
Posts (Atom)